Showing posts with label SIMBA. Show all posts
Showing posts with label SIMBA. Show all posts

Friday, January 12, 2018

Mawingu Tz

Kisa Simba, Julio Ataka Nyumba Oysterbay

Kikosi cha timu ya Simba.
BAADA ya Simba kuonekana kusuasua ka­tika mechi za hivi karibu­ni, Kocha Mkuu wa Dodoma FC, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amefun­guka kama timu hiyo itamuhi­taji yuko tayari kwenda kuwa kocha mkuu lakini atahitaji apewe nyumba ya kisasa eneo la Oysterbay.

Hii ni baada ya kuwepo taarifa kuwa Simba inahitaji huduma ya kocha huyo ambaye kwa sasa anainoa timu hiyo ya Ligi Daraja la Kwanza.

Julio alisema kuwa Simba kama kweli inamuhitaji inatakiwa kufuata yale ambayo anayahitaji yeye na siyo kinyume cha hapo.

“Simba wakitaka mimi nikafundishe timu yao sina tatizo lakini ni lazima wafuata yale ambayo nataka, kwanza wanipe ukocha mkuu, pili nyumba ya kisasa mae­neo ya Oysterbay, gari na hudumu zote ambazo wale makocha Wazungu wakija wanapewa.
“Pia wanapaswa kujua wakinipa hiyo kazi sitaki ku­ingiliwa kwenye kazi yangu mimi pamoja na benchi la ufundi kila watu watambue majukumu yao hapa ndipo timu inaweza kuwa na nafasi ya kufanya vizuri,” alisema Jamhuri.

Tuesday, January 9, 2018

Mawingu Tz

Alichosema Masoud Djuma Baada Ya Kina Mkude Na Kichuya Kutoonekana Benchi...


Alichosema Masoud Djuma baada ya kina Mkude na Kichuya kutoonekana Benchi baada ya kufanyiwa sub.
Jana story kubwa ilikuwa ni Simba kutolewa michuano ya Mapinduzi lakini story nyingine ikaibuka katikati yake kufuatia baadhi ya wachezaji wa Simba kutoonekana katika benchi mara baada ya kutolewa(Kufanyiwa sub) na badala yake kuonekana wamekaa maeneo mengine kabisa ya uwanja wakifatilia mechi.
Masoud Djuma msomaji  ni kocha msaidizi anayeiongoza Simba amewatetea kina Mkude na Kichuya kwa kusema kuwa yeye ndiye aliyewaruhusu wachezaji hao kuondoka katika benchi mara baada ya kuwafanyia mabadiliko.
Masoud amesema wachezaji hao walikuwa wamechoka na hivyo aliwaruhusu waende wakafanyiwe massage vyumbani na hakukuwa na ulazima kwa wao kurejea benchi na wala siyo Tatizo la Nidhamu kama ambavyo wengi walitafsiri.
Katika mchezo huo kati ya Simba na URA kutoka nchini Uganda Simba ilifanya mabadiliko kwa kuwatoa wachezaji Shiza Kichuya, Nicolas Gyan, Jonas Mkude, Mzamiru Yassin na Mwinyi Kazimoto na nafasi zao kuchukuliwa na Mo iBRAHIM, James Kotei, Yusuph Mlipili, Laudit Mavugo na Said Hamis Ndemla.
Simba katika mchezo huo alihitaji ushindi ili kujihakikishia kufuzu katika hatua ya nusu Fainali ya michuano hiyo ya Mapinduzi lakini aliishia kufungwa bao moja pekee bao likipatikana kipindi cha kwanza mara baada ya mchezaji Deboss Kalama kuwahadaa mabeki wa Simba na Kuachia Shuti kali lililomshinda kipa Emmanuel Mseja.
Nusu Fainali zitachezwa kesho Jumatano kati ya Yanga na URA na Azam na Singida United katika uwanja wa Amani Zanzibar.


Mawingu Tz

Niyonzima Arejesha Matumaini Simba

WAKATI wenzake wakiwa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi huko visiwani Zanzibar, kiungo mchezeshaji wa Simba, Mnyar­wanda, Haruna Niyonzima yeye yupo jijini Dar es Salaam akiendelea kujifua ufukweni.
Mnyarwanda huyo alibaki Dar ku­tokana na majeraha ya enka anayoen­delea kuyauguza yaliyomuweka nje ya uwanja kwa muda wa wiki mbili.
Kiungo huyo, alipata majeraha hayo akiwa kwenye mazoezi ya timu hiyo wakati kikosi hicho kikiwa na Mcam­eroon, Joseph Omog aliyesitishiwa mkataba wake hivi karibuni kabla ya msaidizi wake Mrundi, Masoud Djuma kukabidhiwa.
Akizungumza na Championi Ju­matatu, Niyonzima alisema ameanza programu hiyo ya kukimbia ufukweni kwa ajili ya kuiponyesha enka hiyo ili ipone kabisa.
Niyonzima alisema, wakati akien­delea na matibabu mengine atafanya mazoezi ya ufukweni kwani mchanga ni sehemu ya tiba kwa ajili ya jeraha hilo la enka linalomsumbua.
Aliongeza kuwa, hataki kuona akiendelea kusumbuka na jeraha hilo ambalo mara kwa mara linamtokea ili atakaporejea uwanjani lisijirudie.
“Mimi nipo Dar na sipo na timu Zan­zibar, kama unavyofahamu bado enka inanisumbua na hivi sasa nipo nafanya mazoezi ya kukimbia ufukweni huku nikiendelea kupata matibabu mengine hospitali.
“Na mazoezi haya ya ufukweni nayo ni sehemu ya tiba kwangu, kwani mchanga nao ni tiba kwa jeraha hili la enka inayonisumbua kwa muda mrefu,” alisema Niyonzima aliyetua kuichezea Simba katika msimu huu.
Mawingu Tz

Manara Alia Na Mapinduzi Cup Ashindwa Kujizuia, Atoa Mazito.

Baada ya klabu ya Simba kupokea kipigo cha pili katika michuano ya kombe la Mapinduzi kutoka kwa watoza Ushuru wa Uganda ( URA) Cha goli 1-0 Afisa habari wa klabu hiyo,Haji Manara amesema hana neno linaloweza kutosha kuelezea kilichotokea uwanjani.
Aidha amesema kuwa anayajua maumivu wanayopata mashabiki wa timu hiyo kwani yeye ni Msemaji lakini shabiki wa klabu hiyo.
“Kila sentesi niliyoandika nimefuta, hakuna neno linalotosha kuelezea hisia zangu kwa kilichotokea leo Amaan Stadium..nayajua maumivu ya wanasimba….shida yangu mimi ni msemaji kisha shabiki wa hii timu..najua sana pain yenu…but lazma maisha yasonge mbele…
🙏🙏
”>>>Manara


Mawingu Tz

Kisa Kipigo Cha URA, Omog Aivuruga Simba

Kung’olewa kwa Simba katika michuano ya Kombe la Mapunduzi baada ya kuchapwa bao 1-0, kumezua mjadala mpya kuhusiana na Kocha Joseph Omog.
Omog raia wa Cameroon, alifungashiwa virago vyake na uongozi wa Simba ambao ulitumia maneno matamu kusema wamekubaliana aondoke baada ya kuvuliwa ubingwa wa Kombe la Shirikisho na Green Worries inayoshiriki ligi daraja la pili. Lakini baada ya kipigo cha leo, mashabiki wameanza kuhoji kama ilikuwa sahihi kumuondoa Omog.
Baadhi ya mashabiki wa Simba na wa timu nyingine wameeleza kuwa Simba ilikurupuka kumuondoa kocha huyo. Lakini wako waliosema tatizo kubwa ni wachezaji wenyewe ambao wameshindwa kujituma na kuonyesha wanataka kushinda.
Pia kuna mashabiki ambao wameelekeza lawama zao moja kwa moja kwa Kocha Irambona Masoud Djuma kwamba mfumo wake unaonekana kuwa mgumu na si imara katika ulinzi.
Kipigo hicho leo kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar kimekuwa cha pili mfululizo kwa Simba. Mechi iliyopita, Simba ilikutana na kipigo kama hicho kutoka kwa Azam FC na matumaini yao kuendelea ilikuwa leo dhidi ya URA. Bao la URA lilipatikana dakika za nyongeza za kipindi cha kwanza na kipindi chote cha pili, Simba ilishindwa kupata angalau bao moja.

Monday, January 8, 2018

Mawingu Tz

Masikini Aveva; Hali Yake Si Nzuri, Juhudi Zafanyika Kumhamishia Muhimbili Kwa Matibabu Zaidi


Masikini Mwenyekiti wa Simba! Maana hali ya afya ya Rais wa Simba, Evans Aveva bado siyo nzuri kwani jana jioni ndugu na marafiki wa karibu walikuwa kwenye mipango ya kumhamishia Hospitali ya Muhimbili.

Aveva jana alikimbizwa kwenye Hospitali ya Temeke, Dar baada ya hali yake kubadilika akiwa mahabusu kwenye Gereza la Keko.

Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, wanakabiliwa na tuhuma za kughushi nyaraka za klabu hiyo na kutakatisha dola 300,000 (zaidi ya Sh 650 milioni) na wamekuwa rumande tangu Juni 29, mwaka jana.

Taarifa zinaeleza, familia na marafiki wa Aveva walikuwa na mazungumzo na Jeshi la Magereza kwa ajili ya kuomba uhamisho wa hospitali kutokana na aina ya matibabu anayoyapata Hospitali ya Temeke.

Mtoa taarifa huyo alisema, rais huyo anahitaji kupatiwa matibabu mazuri yatakayoendana na ugonjwa ambao ni siri ili apate nafuu arejee katika hali yake ya kawaida.

“Aveva jana (juzi) asubuhi hali yake ilibadilika na kusababisha akimbizwe kwenye Hospitali ya Temeke kwa ajili ya kupata matibabu ya afya yake.

“Lakini wakati akiendelea na matibabu Temeke, baadhi ya ndugu na marafiki wamejaribu kuliomba Jeshi la Magereza kwa ajili ya kupata ruhusa ya kumhamishia Hospitali ya Muhimbili kwa ajili ya kupata matibabu mazuri,” alisema mtoa taarifa huyo.


Alipotafutwa Kaimu Makamu wa Rais wa timu hiyo, Idd Kajuna kuzungumzia hilo, simu yake ya mkononi haikuwa ikipokelewa, lakini alipotafutwa Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa timu hiyo, Hajji Manara kuzungumzia hIlo, alisema: “Mimi nipo Zanzibar sifahamu chochote kuhusiana na taarifa hizo, naomba waulize watu waliopo Dar.”

SOURCE: CHAMPIONI

Saturday, January 6, 2018

Mawingu Tz

Ishu Ya Okwi Kugoma Kurejea Kisa Kuwadai Simba,Simba Wafunguka Haya

ISHU YA OKWI KUGOMA KUREJEA KISA KUWADAI SIMBA,SIMBA WAFUNGUKA HAYA
Klabu ya Soka ya Simba ya Jijini Dar es Salaam imekanusha vikali taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya Habari kuwa klabu hiyo imeshindwa kuwalipa fedha za usajili baadhi ya wachezaji wake.
Baadhi ya vyombo vya habari vimewataja wachezaji hao kuwa ni Emmanuel Okwi na Asante kwasi kuwa hawatacheza hadi walipwe fedha zao za usajili, jambo ambalo Simba imesema si la kweli.
Simba imesema taarifa hizo zimejikita kwenye kuharibu taswira ya klabu, na yenye nia ovu kwa timu ya Simba ambayo ipo kwenye mashindano ya kombe la Mapinduzi yanayoendelea huko Zanzibar kwa sasa.
-Simba inapenda kuwaambia wanachama na washabiki wake kuwa, haidaiwi na mchezaji yoyote pesa yoyote si tu ya usajili hata za mishahara,” imesema taarifa hiyo.
Okwi ataonekana hivi karibuni.
-Tupende pia kuwaarifu mchezaji Emmanuel Okwi ataonekana uwanjani hivi karibuni baada ya ruhusa yake ya matibabu kumalizika, huku Kwasi akiendelea kuitumikia klabu kama mlivyoona kwenye mchezo dhidi ya Jamhuri toka kisiwani Pemba,” Ilisema taarifa hiyo iliyoandikwa na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Haji Manara.
Ikumbukwe mlinzi Asante Kwasi alikuwapo kwenye kikosi kilichocheza na Jamhuri ya Zanzibar katika michuano ya Mapinduzi na kufanikiwa kufunga bao la tatu katika ushindi wa mabao 3-1.
Mawingu Tz

Kikosi cha Simba Dhidi Ya Azam Fc Leo 06.01.2018

SIMBA SC LINE UP – MAPINDUZI CUP 06.01.2018.
1.Emanuel Mseja- 30
2.Nicholas Gyan – 29
3.Mohamed Hussein- 15
4.Juuko Murshid-06
5.Asante Kwasi- 16
6.Jonas Mkude – 20
7.James Kotei- 03
8.Yassin Mzamiru -19
9.John Bocco – 22
10.Said Hamisi – 13
11.Shiza Kichuya-25

SUBS.
1. Ally Salim- 31
2.Jamali Mwambeleko- 26
3.Yusufu Mlipili – 05
4. Erasto Nyoni – 18
5.Paul Bukaba-23
6.Mohamed Ibrahim- 04
7.Mwinyi Kazimoto -24
8.Laudit Mavugo -11
9.Moses Kitandu-35
Mawingu Tz

Aishi Alivyoachana Na Ukapera Kwa Kufunga Ndoa Na Aisha


Kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula ameachana na ukapera baada ya kufunga ndoa na mpenzi wake wa siku nyingi aitwaye Aisha.

Manula hakwenda Zanzibar ambako Simba inashiriki michuano ya Kombe la Mapinzudi ili kukamirisha kazi hiyo ya kuuaga ukapera.

Taarifa zinaeleza, Aishi na Aisha wamekuwa wapenzi wa siku nyingi.
Mawingu Tz

Kwasi: Nitawafunga Mpaka Mkome

WAKATI Kaimu Kocha wa Simba, Masoud Djuma, akiamini Asante Kwasi atawasaidia kutwaa mataji msimu huu, beki huyo amepania kufanya mambo makubwa zaidi hasa kufunga mabao muhimu.

Usiku wa kuamkia jana Ijumaa, Kwasi aliifungia Simba bao moja katika ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi dhidi ya Jamhuri kwenye Uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar.

Kwasi raia wa Ghana aliichezea Simba kwa mara ya kwanza baada ya kusajiliwa katika usajili wa dirisha dogo Desemba mwaka jana akitokea Lipuli FC ya Iringa. Msimu uliopita Kwasi alichezea Mbao FC.
Beki huyo aliliambia Championi Jumamosi kuwa: “Nimejisikia furaha kufunga bao lile katika mechi yangu ya kwanza, na naamini nitaendelea kufunga zaidi na kuisaidia timu yangu kufanya vizuri kwenye michuano hii.
“Najua kiu ya mashabiki ni kuniona nafanya yale niliyokuwa nayafanya katika timu niliyotoka awali, kazi ni kuzuia pia kufunga mabao muhimu kwa timu yangu.

“Nitaendelea kupambana kuhakikisha Simba inafanya vizuri si kwenye michuano hii pekee, bali hata kwenye michuano mingine ambayo tunashiriki msimu huu.”
Naye Kaimu Kocha wa Simba, Djuma ameonyesha kunogewa na uwezo wa Kwasi kiasi cha kusema, beki huyo atawapa mataji msimu huu.
Djuma ametoa kauli hiyo kutokana na ukweli kwamba, Kwasi ameonyesha uwezo mkubwa wa kulinda lango na kufunga mabao ndani ya wakati mmoja.
“Katika timu yangu nataka kuona kila mchezaji anafunga mabao bila ya kuangalia beki au kiungo
kwani kazi ya kufunga siyo ya washambuliaji peke yake, naamini uwezo mkubwa wa kufunga wa Kwasi licha ya nafasi anayocheza.
“Ujio wa Kwasi katika timu yetu kutaisaidia timu yetu kupata makombe, kwani tofauti na uwezo wake kulinda na kuokoa hatari golini ana uwezo wa kufunga mabao.
“Alitufunga wakati akichezea Lipuli na hapa amefunga, huyu ni mtu muhimu pia nimefuatilia rekodi yake akiwa Mbao FC kabla ya kwenda Lipuli alikuwa akifunga mabao,” alisema Djuma.
Kwasi leo anaichezea Simba dhidi ya Azam FC kwenye mechi ya Kundi A la Kombe la Mapinduzi.

Tuesday, January 2, 2018

Mawingu Tz

Kikosi cha Simba kinachoanza dhidi ya Mwenge leo saa kumi


Kikosi cha Simba kitakachoanza leo dhidi ya Mwenge
1.Emanuel Mseja- 30
2.Paul Bukaba – 23
3.Mohamed Hussein- 15
4.Yusufu Mlipili-05
5.Asante Kwasi- 16
6.Jonas Mkude – 20
7.Ally Shomari- 21
8.Said Hamisi -13
9.Juma Luizio – 10
10.Moses Kitandu – 35
11.Jamali Mwambeleko-26

SUBS.
1. Ally Salim- 31
2.Erasto Nyoni – 18
3.Shiza Kichuya -25
4. Kelvin Faru – 40
5.John Bocco -22
6.Nicholas Gyan -29
7.Mohamed Ibrahim – 04
Mawingu Tz

Mashabiki Wa Simba Bhana CHeki Walichokisema Kuhusu John Bocco

Unaweza kusema mashabiki wa soka hawana kauli moja baada ya baadhi yao kumsifia mshambuliaji wa Simba, John Bocco kuwa anajituma sana.

Baada ya Bocco kufunga mabao mawili wakati Simba ikiimaliza Ndanda FC kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, mashabiki hasa wa Simba wanaonekana kufurahishwa na mwendo wa Bocco.
Katika mijadala ya makundi mbalimbali pia kupitia mtandao wa Instagram, mashabiki hao wa soka wameonyesha kufurahishwa na Bocco.

Wengi wameeleza pamoja na kufunga lakini amekuwa akicheza kwa juhudi kubwa na inapaswa kuwa mfano kwa wengine,
Lakini wako waliosema, Bocco anaonekana ana malengo hata kuliko wachezaji wengi wa kigeni kwa kuwa hataki kufeli.
Wakati wakimwagia sifa kibao, siku chache zilizpita, mashabiki walikuwa wakilalama kwamba Bocco anaonekana kutokuwa na msaada.


Mara kadhaa, hadi uwanjani walikuwa wakipiga kelele kutaka Bocco ataolewe, madai kwamba hana msaada.
Mawingu Tz

Obrey Chirwa Mbioni Kutua Simba

Ni Kauli ambayo unaweza ukaisema kutokana na Hali iliyopo kwasasa kati ya Yanga na Straika wao kutoka nchini Zambia Obrey Chirwa.
Kulingana na Gazeti la dimba la Leo limeeleza kuwa Obrey Chirwa huenda akatua Msimbazi timu ya Simba endapo tu Yanga watashindwa kumtimizia mahitaji yake anayoyata kwasasa.
ISHU YA KUWADAI YANGA
Inadaiwa kuwa Yanga bado wanadaiwa na Obrey Chirwa ambaye kwa msimu huu amekuwa mchezaji muhimu sana upande wa Ushambuliaji kiasi cha Kugeuka kuwa Tegemezi eneo la Ushambuliaji.
Inadaiwa Chirwa ambaye alitarajiwa kutua Nchini siku ya Jumamosi kuja kwake Tanzania hakuja kwaajili tu ya Kucheza bali kufanya mazungumzo juu ya hatma ya madai yake.
MKATABA WAKE YANGA WAELEKEA MWISHONI
Mkataba kati ya Chirwa na Yanga  unaelezwa kuwa Uko mbioni kuisha kwani utaisha mwishoni mwa Msimu huu wa Ligi hivyo basi imesalia chini ya miezi 6 hivyo Upande wa Pili wa Simba unaotajwa kutoa Udenda Juu yake huenda ikawa rahisi kuanza kufanya naye maongezi mapema ili kumsajili kwaajili ya michuano ya kitaifa na Kimataifa.
ANATAKA DAU KUBWA ILI AONGEZE MKATABA YANGA
Taarifa za Ndani kutoka Yanga  zinadai Kuwa Chirwa anataka alipwe Shilingi milioni 120 ili Kuongeza Mkataba Yanga kutokana na kuongezeka kiwango chake msimu huu, Wakati hali ya Uchumi ndani ya Yanga inaelezwa kuwa siyo nzuri sana
YANGA NAO HAWATAKI MCHEZO KWENYE HILI
Klabu ya Yanga kwa upande wao inasemekana wapo katika mipango ya kuhakikisha wanamalizana na Chirwa mapema kabla hata muda wake haujaisha wa mkataba ili yasije kuwakuta kama yaliyowakuta kwa Niyonzima.
Hivyo wanasubiri waweke mambo sawa kisha wakae mezani na Chirwa ili kuangalia uwezekano wa Chirwa kuongeza makataba mapema.

Thursday, December 28, 2017

Mawingu Tz

Yanga Sc Waiwangia Simba Mchana Kweupee


HUENDA kauli hii ikawa na ukakasi mkubwa kwa mashabiki wa Simba lakini ndiyo hivyo tena, kwamba wameambiwa na wenzao wa Yanga kuwa kama wanataka ubingwa wowote inabidi basi wasubiri msimu ujao wa 2018/19, kwani msimu huu hawana chao.
Yanga wamefikia kutamka maneno hayo mazito baada ya kuwaona watani zao hao wa jadi wakitupwa nje ya michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC), wakikubali kichapo cha mabao 4-3 kutoka kwa Green Warriors kwa mikwaju ya penalti.
Simba ndio waliokuwa mabingwa watetezi wa michuano hiyo lakini wakajikuta wakipata aibu hiyo ya mwaka, kitendo kilichowafanya kuamua kumtimu kocha wao mkuu Joseph Omog na sasa wanahaha kutafuta mbadala wake.
Wakati Simba wao wakiangukia pua, watani zao hao wa jadi mwishoni mwa wiki iliyopita walijihakikishia kusonga mbele hatua inayofuata baada ya kuwashushia kipigo cha mabao 2-0, Reha FC ya Temeke mchezo uliochezwa Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.
Kitendo hicho kimewafanya Yanga kukenua wakijiapiza kwamba msimu huu watakomba makombe yote na kama Simba wana hamu ya kunyakua ubingwa wowote, wanatakiwa kusubiri mpaka msimu ujao wa 2018/19 kwani msimu huu una wenyewe.
Msimu wa 2016/17, Yanga walifanikiwa kunyakua makombe yote, yani lile la Azam maarufu kama FA na la Ligi Kuu na sasa wanasema msimu huu tena watafanya hivyo kitu ambacho kinawafanya Simba kuweweseka hasa baada ya kuutema ubingwa wao wa FA.
Kitu pekee kinachoweza kuwabeba Simba kushiriki michuano ya kimataifa msimu ujao ni kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu msimu huu, lakini Yanga wamesema wanataka kutetea ubingwa wao, yaani wautwae mara ya nne mfululizo na kuvunja rekodi hiyo ikimaanisha Wekundu wa Msimbazi, wana mlima mrefu wa kupanda.
Baada ya mchezo dhidi ya Reha kumalizika, kocha msaidizi wa Yanga, Shadrack Nsajigwa, alisema malengo yao ni kuhakikisha msimu huu wanawafurahisha tena mashabiki wao kwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu na ule wa FA.
“Kwanza niwashukuru wachezaji wetu kwa jinsi walivyopambana mpaka kupata ushindi huu wa mabao 2-0, nadhani lengo letu ni kuhakikisha msimu huu tunafanya vizuri na kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu na hili Kombe la FA,” alisema Nsajigwa, kauli ambayo si nzuri kwa mashabiki wa Simba.
Mbali na kauli hiyo ya Nsajigwa, idadi kubwa ya mashabiki na wanachama wa kikosi hicho, wameshajihakikishia kwamba, Simba hawawezi kufanya lolote mbele ya timu yao.
“Simba kwishnei kabisa, yaani msimu huu watasubiri sana, wao kama wanataka ubingwa wasubiri msimu ujao wa 2018/19 kwani msimu huu Yanga tutaendelea kutesa, wameshatolewa kwenye kombe lao la FA, tena wakifungwa na timu ndogo sasa ndiyo Ligi Kuu wataweza,” walisikika wakisema mashabiki wa Yanga baada ya kushinda mchezo wao dhidi ya Reha FC.
Hata mitaani kwenye vijiwe mbalimbali mashabiki wa Yanga wanaamini Simba wamepoteza dira hasa kitendo cha kumtimua kocha wao mkuu, Joseph Omog, kinatajwa kwamba kutazidi kuwavuruga.
Yanga wanaamini watashinda michezo yao yote ya Ligi Kuu iliyobakia ikiwamo wa mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Mbao FC, utakaochezwa Uwanja wa CCM Kirumba, jijini Mwanza, huku wakiamini Simba wataanza kupoteza dira dhidi ya Ndanda FC na kushuka kileleni.
Mawingu Tz

Masoud Djuma Atoa Ya Moyoni Kuhusu Omog

Aliyekuwa kocha wa Simba Mcameroon, Joseph Omog.
KOCHA aliyeachiwa mikoba ya aliyekuwa kocha wa Simba Mcameroon, Joseph Omog, Mrundi Masoud Djuma, amesema kuwa anasikitishwa na kitendo cha kuona kocha huyo akiondoka huku wakiwa hawajamaliza jukumu lao la kuhakikisha wanaipa ubingwa klabu hiyo. Omog alifungashiwa virago vyake  wikiendi iliyopita baada ya kuiongoza Simba katika mechi  52 kati ya hizo ameshinda michezo 35, sare 11 na akifungwa michezo sita tu.

Championi Jumatano limepata nafasi ya kuzungumza na Masoud Djuma, lengo ni kujua muda mfupi atamisi nini kutoka kwa Omog ambaye wam e i s h i kwa muda mfupi.
CHAMPIONI: UTAKUMBUKA NINI KUTOKUWEPO KWA OMOG? DJUMA:
“Kama nimeishi na mtu vizuri kwa muda huu mfupi bila tatizo naye, nasikitika kumkosa maana nje na kazi tayari alikuwa akinichukulia mimi kama mtoto wake. “Wakati naanza kazi hapa Simba nilikuwa na matatizo yangu makubwa ambayo hakuna mtu mwingine yeyote niliyemueleza zaidi yake, lakini alinishauri kiasi kwamba niliona kama nipo nyumbani.

“Mbali na hivyo utaona ilifikia kipindi hata nikiwa na njaa nikitaka kununua hata mkate alikuwa ananizuia kulipa kama yupo karibu analipa yeye na anasema mimi ni mwanaye, hivyo sina haja ya kuhangaika mbele yake. “Kwa maana hii nasikitishwa sana na kuondoka kwake maana nitamisi mambo mengi kutoka kwake kwani kulikuwa kuna vitu namueleza yeye mwingine siwezi na alinivumilia sana.
Mrundi Masoud Djuma (katikati) akiongea na wanahabari.
CHAMPIONI: TAYARI UONGOZI UMEMTEMA JE, UTAWEZA KUENDELEZA USHINDANI UWANJANI BILA YEYE? DJUMA:
“Ameniachia jukumu kubwa sana na ukiangalia nina mechi kubwa na muhimu mbele yangu dhidi ya  Ndanda itakuwa ni moja ya mtihani wangu mgumu sana hivyo ninajipanga ili nisije kuanza kuleta kelele mpya.

“Timu ina presha kubwa kwa kila aliye mbele yetu kutokana na kuondoka kwa Omog ambaye naamini kuna waliomchukia na waliompenda hivyo kazi yangu sasa ni kuhakikisha nawaunganisha kuwa kitu kimoja.

“Hata mimi kuna wanaonipenda na wasionipenda hivyo jukumu langu sasa ni kupambana kadri ya uwezo wangu kuhakikisha nawaweka sawa ili huko mbele mambo yaweze kuwa mazuri tofauti na matarajio ya wanaotuombea mabaya.

CHAMPIONI: UMEJIFUNZA NINI KUTOKA KWA OMOG? DJUMA:
“Yapo mengi niliyojifunza kwake, la kwanza kubwa kuunganisha upendo ndani ya timu, pili wakati nakuja hapa pamoja na kwamba huko Rwanda nilikuwa kocha mkuu, baada ya kuitwa hapa Simba niliamua kuja kujifunza mambo mengi kutoka kwa Omog ambaye nilikuwa nikiamini kutokana na ukongwe wake hii fani.

“Lakini hata uzoefu wake kwenye ligi hii ya hapa Tanzania kwani amefundisha muda mrefu, kwa kuwa tayari niliamua kuja Simba na nikijua yupo yeye sikuangalia sana suala la madaraka ya ukocha mkuu zaidi ya kuangalia elimu niliyotarajia kuipata kutoka kwake.

“Jambo ambalo wengi walikuwa hawalifahamu maana kuna wale ambao walidhani mimi nipo hapa kutaka kuwa kocha mkuu tu na si kujifunza mengi ambayo nimeyapata kutoka kwake na kwamba nitammisi sana kwa sababu nilikuwa bado nahitaji elimu yake nzuri”.

CHAMPIONI: UNAWASHAURI NINI VIONGOZI JUU YA KUONDOKA KWA OMOG?
DJUMA: “Sina hata cha kushauri hapo kwani hata niseme nini ni ngumu kubadili hisia za wengi. Kwa wema alionifanyia mimi ningependa kuendelea kuwa naye tu lakini kwa kuwa kazi yetu hii ina changamoto kila ulipo maana siku zote timu ikifanya vizuri ni ya wote, ikifeli ya kocha.

“Ujue wakati nakuja kwa mara ya kwanza waandishi waliniuliza nimejipanga vipi na kutimuliwa hapa Simba, ila jibu langu siku hiyo niliwaambia kuwa kutokana na presha ya mpira inavyokuwa siku zote ukiwa kama kocha lazima ukiitwa sehemu unatakiwa kufungua begi lako nusu kwa muda wowote safari inaweza kukuta hivyo ili hata Omog alikuwa analijua vilevile kwangu linaweza kutokea muda wowote ule.

“Natambua changamoto nyingi sana kwenye mpira kwani utagundua kabla sijakuwa kocha mkuu huko Rwanda niliwahi kuwa kocha msaidizi kwenye timu ya vijana ya Burundi, hivyo nina uzoefu wa mambo mengi uwanjani na nje ya uwanja.

CHAMPIONI: UNAJISIKIAJE KUACHIWA SIMBA HUKU UKIWA KILELENI?
DJUMA: “Ninaona kama mtihani mkubwa sana kwangu kwani Simba ni timu kubwa na ina mashabiki wengi kupita wale wa Rayon, japo presha kwa watu wa mpira  huwa ni ileile.

“Simba wao wanahitaji ushindi kila siku na si kingine, kwa maana hiyo naona kama naingia kwenye mtego ila kwa kuwa Mungu ndiye kiongozi wa kila jambo hakika nitashinda tu kuanzia mechi iliyopo mbele yangu ili tuzendelee kuongoza ligi hii.”

“Mpira lazima uwe na ushirikiano kwa watu wote yaani kuanzia kocha, wachezaji na uongozi kwa ujumla kwani ili matokeo yapatikane baraka za kila mtu ndani ya timu ziweze kutumika hivyo mkiwa pamoja hata kutegemea kumtupia lawama kocha tu huwa kunapungua japo najua ipo siku moja hata mimi nitaondoka kwa kutupiwa mzigo huo kwani timu ikifanya vibaya ni ya kocha pekee.
Mawingu Tz

Umesikia Alichokisema Kwasi? Atoa Kali Ya Funga Mwaka Simba


BEKI Mghana, Asante Kwasi, amewaambia mashabiki wa Simba kwamba hakwenda katika kikosi chao kuuza sura, bali ni kuwafanyia kazi ambayo itawafanya wasijute kumsajili.
Kwasi ametua Simba katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo akitokea Lipuli ya Iringa, japo uhamisho wake ulikumbwa na bonge la zengwe.
Baada ya tetesi za Simba kumsajili Kwasi kuzagaa nchini, Lipuli walikuja juu wakisisitiza mchezaji huyo kuwa mali yao, akiwa bado hajafikisha muda wa kufanya mazungumzo na klabu yoyote ile bila kuwasiliana nao kama walivyofanya Wekundu wa Msimbazi hao.
Kwa mujibu wa kanuni za usajili, mchezaji yeyote anaweza kufanya mazungunzo na klabu nyingine inayomtaka iwapo tu atakuwa amebakiza si zaidi ya miezi sita katika mkataba na klabu yake.
Baada ya kubaini ‘walibugi’, Simba walikubali yaishe kwa kukutana na uongozi wa Lipuli na mwisho wa siku, kukubaliana na kumtwaa kwa dau la Sh milioni 25.
Akizungumza na BINGWA jana, Kwasi alisema amefurahi mno kutua Simba, kwani ni klabu aliyokuwa amepania mno kuitumikia hapa nchini.
Aliwataka mashabiki wa timu hiyo kumpa sapoti ya kila aina ili aweze kutimiza majukumu yake kadiri ya uwezo wake, akiamini ana uwezo wa kuongeza kitu ndani ya kikosi hicho.
“Nawaomba mashabiki wa Simba, wanisapoti na kuniamini, naahidi kutimiza majukumu yangu ambayo yamenipeleka hapo, nitatumia uwezo na juhudi zangu zote, kikubwa ni ushirikiano wao na kwa uwezo wa Mungu, kila kitu kitafanikiwa,” alisema Kwasi.
Akiizungumzia safu ya ulinzi katika kikosi chake hicho kipya, alisema anatambua anakwenda kukutana na wachezaji wazuri lakini atapambana kuhakikisha anapata nafasi kwenye kikosi cha kwanza.
Katika safu hiyo ya ulinzi, Kwasi anakwenda kukutana na akina Salim Mbonde, Jjuuko Murushid, Yusuph Mlipili na Paul Bukaba, ambapo atatakiwa kukaza buti ili kumshawishi kocha amuamini na kumpanga kikosi cha kwanza.

Wednesday, December 27, 2017

Mawingu Tz

Taarifa Mpya Kutoka Simba Mchana Huu

Klabu ya Simba mchana huu Imetoa taarifa juu ya safari yao kwenda Mtwara ambapo inatarajia kucheza dhidi ya Ndanda kutoka Mkoani Humo.
Kikosi na msafara mzima wa Simba  unatarajia kuondoka kesho Alfarjiri kuelekea Mtwara kwaajili ya Mchezo dhidi ya Ndanda Jumamosi December 30, 2017

Mawingu Tz

Simba Yawatupa Jukwaani Okwi, Niyonzima

KOCHA wa Simba, Masoud Djuma amesema kuwa kutokana na mshambuliaji wake, Emmanuel Okwi raia wa Uganda kutokuwa sawa, amelazimika kumpatia mazoezi ya peke yake ili kumuweka fiti huku akitarajiwa kukosa mechi dhidi ya Ndanda mchezo ambao pia ataukosa Haruna Niyonzima.
Haruna Niyonzima.
Okwi alipatwa na majeraha ya enka hivi karibuni katika mechi dhidi ya Mbeya City ambapo bado anaendelea na matibabu. Akizungumza na Championi Jumatano, Masoud alisema kuwa, Okwi bado hayupo fiti hivyo amemua kumpatia programu maalumu ya kumweka fiti kutokana na majeraha yake ili aweze kurejea katika kiwango chake.

“Okwi bado hayupo fiti na hajaanza mazoezi pamoja na wenzie kwa sasa kuna mazoezi nimempatia ambayo anayafanya peke yake ya kuzunguka uwanja pamoja na viungo huku akiendelea kuwa karibu na dokta kwa lengo la kuangalia afya yake.

“Siwezi kumtumia mchezaji akiwa bado hajapona vyema kwani nitaweza kumuongezea majeraha zaidi na kuharibu uwezo wake, hivyo sitarajii kumtumia dhidi ya Ndanda hadi hapo atakapofanikiwa kuwa fiti. “Ukiachana na yeye pia kuna Niyonzima hayupo sawa, lakini kwa upande wa wachezaji wengine wapo fiti, tunahitaji kushinda mchezo wetu huo,” alisema Djuma.
Mawingu Tz

Taarifa Mpya Kutoka Simba Asubuhi Hii Dec 27 2017

Beki na kiungo kiraka mpya wa Simba, Asante Kwasi rasmi ameanza mazoezi akiwa na uzi wa klabu hiyo.

Kwasi aliyewasili jijini Dar es Salaam, jana jioni akitokea Iringa, ameanza mazoezi kwenye ufukwe wa Coco.

Raia huyo wa Ghana ndiye alikuwa gumzo zaidi wakati Simba ikifanya juhudi za kumsajili na Lipuli FC wakipinga.

Hata hivyo, baadaye timu hizo zilifikia mwafaka na mwisho Kwasi sasa ni mali ya Simba.

Hata hivyo, ili awe mali ya Simba mchezaji huyo ilikuwa ni lazima aonekane katika uzi wa Simba na si ule wa Lipuli ambao wengi walikuwa wakiufananisha na wa Simba.

Tuesday, December 26, 2017

Mawingu Tz

Hatima Ya Straika Wa Msumbiji Katika Kikosi Cha Simba Hii Hapa.

Klabu ya Simba imeamua kuachana na straika mkali wa kuchana nyavu kutoka Msumbiji, Dayo Antonio Domingos na badala yake kumbakisha kikosini Mrundi Laudit Mavungo.
Kwa wanaokumbuka mchana wa Ijumaa ya Desemba 15, straika huyo wa Ferroviario de Beira alitua nchini ikiwa ni saa chache kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo la usajili kabla ya kuongezwa hadi Jumamosi iliyopita.
Straika huyo aliletwa ili kuchukua nafasi ya Mavugo aliyekuwa mbioni kutolewa kwa mkopo Arabuni, licha ya mwenyewe kung’ang’ania kutaka kwenda kucheza soka Kenya katika klabu ama Gor Mahia au AFC Leopards.
Mabosi wa Simba walimkimbiza mbiombio hotelini na kukaa naye faragha ili kumalizana naye kuwahi dirisha la usajili sawia na beki Mghana Asante Kwasi aliyechukuliwa kutoka Lipuli aliyetua Msimbazi kuziba nafasi ya Method Mwajali.
Asubuhi ya siku hiyo ikathibitika kuwa pande hizo mbili zimemalizana na hata picha zikasambazwa, lakini kumbe nyuma ya pazia, mipango ilikwama na ndio maana straika huyo aliamua kutimka kwao kimyakimya.
Ipo hivi. Simba imeshindwa kukamilisha usajili wa straika huyo iliyokuwa imempa mkataba wa miaka miwili baada ya kuchelewa kupata barua ya uhamisho kutoka kwao, hivyo kuamua kuachana naye rasmi.
Habari za uhakika kutoka ndani ya Simba ni kwamba Domingos hatakuwa katika kikosi cha Simba labda mpaka msimu ujao kama wataendelea kumhitaji na badala yake Mavugo anabakishwa kikosini.
“Domingos alikuwa kwenye malengo yetu lakini vibali vyake havikukamilika ndiyo maana tulishindwa kuingiza jina lake kwenye usajili japo ni kweli tulimpa hata mkataba na aliusaini, ndiyo maana Mavugo yupo mpaka sasa, vinginevyo Mavugo tungemwachia ili aende alikotaka, “ alisema mmoja wa vigogo wa Simba aliyeomba kuhifadhiwa jina lake kwa vile hayupo Kamati ya Usajili.
Makamu Mwenyekiti wa Usajili Simba, Kassim Dewji alisema atakuwa na nafasi ya kuzungumzia usajili mzima wa Simba leo, hivyo kushindwa kuweka bayana juu ya Domingos kusepa Msimbazi.