Wednesday, December 27, 2017

Mawingu Tz

Taarifa Mpya Kutoka Simba Asubuhi Hii Dec 27 2017

Beki na kiungo kiraka mpya wa Simba, Asante Kwasi rasmi ameanza mazoezi akiwa na uzi wa klabu hiyo.

Kwasi aliyewasili jijini Dar es Salaam, jana jioni akitokea Iringa, ameanza mazoezi kwenye ufukwe wa Coco.

Raia huyo wa Ghana ndiye alikuwa gumzo zaidi wakati Simba ikifanya juhudi za kumsajili na Lipuli FC wakipinga.

Hata hivyo, baadaye timu hizo zilifikia mwafaka na mwisho Kwasi sasa ni mali ya Simba.

Hata hivyo, ili awe mali ya Simba mchezaji huyo ilikuwa ni lazima aonekane katika uzi wa Simba na si ule wa Lipuli ambao wengi walikuwa wakiufananisha na wa Simba.


Tupe Maoni Yako