Showing posts with label LEAGUE1. Show all posts
Showing posts with label LEAGUE1. Show all posts

Friday, December 15, 2017

Mawingu Tz

Iniesta Atoa Ya Moyoni Kuhusu Suala La Neymar Kwenda Real Madrid

Mshambuliaji  wa Paris Saint- Germain, Neymar.
KIUNGO mkongwe wa Barcelona, Andres Iniesta amesema hana hofu kuhusu Neymar kujiunga na Real Madrid lakini akakiri kuwa ikitokea hivyo haitampendeza kutokana na uhusiano wa Neymar na mastaa wengine wa Barcelona wakati alipokuwa akiichezea timu hiyo.

Iniesta amecheza na Neymar kwa miaka minne kabla ya mchezaji huyo kuondoka na kuhamia Paris Saint- Germain lakini kumekuwa na taarifa za kuwaniwa kwa ukaribu na Real Madrid.
Kiungo mkongwe wa Barcelona, Andres Iniesta.
“Chochote kinaweza kutokea kwenye soka, kuna mambo ambayo yalionekana ni vigumu kutokea na yakatokea, sitashangaa lakini haitapendeza kwa kuwa kwa kuwa ni mchezaji mzuri lakini sina hofu,” alisema Iniesta.

Tuesday, December 12, 2017

Mawingu Tz

Maneno Ya Shombo Ya Wachezaji Man City Kwa Zlatan, Ndiyo Chanzo Cha Ngumi Kavu Man United Vs Man City






Maneno ya shombo ya wachezaji wa Manchester City, ndiyo yaliyosababisha mzozo na wenyewe kutwangana ngumi.

Hali ya wachezaji hao kutoelewana imeelezwa ilisababishwa na kauli iliyotoka katika kundi la wachezaji wa Man City waliokuwa wakipita mbele ya wachezaji wa Man United baada ya kushinda 2-1.

Mmoja wa wachezaji alimueleza Zlatan Ibrahimovic kwamba: “Zlatan, unachonga sana lakini hauna unalofanya.”

Ilikuwa tayari mchezo umeisha na baada ya hapo, ugomvi mkubwa uliibuka na kusababisha Kocha Msaidizi wa Man City, Mikel Arteta kupasuliwa katika paji la uso.


Man City ilifafanikiwa kutoka nyuma na kusawazisha mwisho kupata ushindi wa mabao 2-1.