Tuesday, January 2, 2018

Mawingu Tz

Mashabiki Wa Simba Bhana CHeki Walichokisema Kuhusu John Bocco

Unaweza kusema mashabiki wa soka hawana kauli moja baada ya baadhi yao kumsifia mshambuliaji wa Simba, John Bocco kuwa anajituma sana.

Baada ya Bocco kufunga mabao mawili wakati Simba ikiimaliza Ndanda FC kwa mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara, mashabiki hasa wa Simba wanaonekana kufurahishwa na mwendo wa Bocco.
Katika mijadala ya makundi mbalimbali pia kupitia mtandao wa Instagram, mashabiki hao wa soka wameonyesha kufurahishwa na Bocco.

Wengi wameeleza pamoja na kufunga lakini amekuwa akicheza kwa juhudi kubwa na inapaswa kuwa mfano kwa wengine,
Lakini wako waliosema, Bocco anaonekana ana malengo hata kuliko wachezaji wengi wa kigeni kwa kuwa hataki kufeli.
Wakati wakimwagia sifa kibao, siku chache zilizpita, mashabiki walikuwa wakilalama kwamba Bocco anaonekana kutokuwa na msaada.


Mara kadhaa, hadi uwanjani walikuwa wakipiga kelele kutaka Bocco ataolewe, madai kwamba hana msaada.

Tupe Maoni Yako