Showing posts with label Ratiba&Matokeo. Show all posts
Showing posts with label Ratiba&Matokeo. Show all posts

Tuesday, January 2, 2018

Mawingu Tz

Asante Kwasi Nae Atoa Ya Moyoni Kuhusu Tshishimbi

Asante Kwasi.
BEKI mpya wa Simba, Asante Kwasi, raia wa Ghana, ameibuka na kusema kuwa, katika wachezaji wa Yanga, Papy Tshishimbi ni mfano wa kuigwa kutokana na jinsi anavyomfahamu. Kwasi ambaye aliwahi kucheza na Tshishimbi kwenye kikosi cha Mbabane Swallows ya Swaziland kabla ya msimu uliopita kuibukia Mbao FC, hivi sasa amejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili akitokea Lipuli FC.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Kwasi alisema anachofahamu kutoka kwa Tshishimbi ni mchezaji mtulivu ndani na nje ya uwanja, lakini pia anatimiza majukumu yake ya ndani ya uwanja ipasavyo, hivyo ni mchezaji wa kipekee kikosini hapo.
Papy Tshishimbi.
“Namjua sana Tshishimbi kuliko mchezaji mwingine pale Yanga kwa sababu nimewahi kucheza naye kwenye kikosi cha Mbabane, ni mchezaji mzuri kwani anajua anatakiwa kufanya nini na wakati gani ndani ya uwanja.

Kutokana na hilo, naamini ataisaidia sana timu yake, lakini pia ukimkuta nje ya uwanja, ni mtulivu sana hana ile tabia ya ubabeubabe, hivyo ndivyo ninavyomfahamu huyo jamaa,” alisema Kwasi.

Saturday, December 23, 2017

Mawingu Tz

Vikosi Kamili Vinavyoanza Game Ya Real Madrid Na Barcelona Hivi Hapa



Mawingu Tz

USAJILI : Mido La Kutisha Lililoyetinga "first eleven" CECAFA Laitaja Yanga

USAJILI : Aliyetinga ” first eleven ” CECAFA aitaja Yanga
Kiungo wa timu ya Taifa ya Zanzibar ” Zanzibar Heroes ” Abdulaziz Makame amefunguka Juu ya kama Yanga wanamwitaji kumsajili na Kusema yeye yuko tayari.
Makame aliyeng’ara sana kwenye michuano ya CECAFA yaliyofanyika mapema mwezi Huu (December ) nchini Kenya katika miji ya Machakos na Kisumu kiasi cha kuvutia timu nyingi
Makame msomaji wa Kwataunit.com amesema yeye yuko tayari kucheza Yanga na kama kweli Yanga wanamtaka basi hata leo hii yeye yuko tayari kucheza timu hiyo.
Abdulaziz Makame alikuwa moja kati ya wachezaji waliochaguliwa kwenye kikosi bora cha mashindano ya CECAFA 2017 kutokana na kucheza mechi zote katika ubora wa hali ya Juu.
Hata hivyo katibu mkuu wa Yanga Boniface Mkwasa siku kadhaa zilizopita aliiambia kwataunit.com kuwa baada ya kumsajili Mkomola na Kayembe hawana mpango wa Kuongeza mchezaji mwingine ndani ya Kikosi chao.
Mawingu Tz

Video:Magoli Yote Green Worriors Vs Simba sc Na Penati



Mawingu Tz

Arsenal 3-3 Liverpool, Lilikuwa Bonge La Game Wabovu Watupu Walivyokutana, Picha Hizi Hapa...



Arsenal (4-3-3): Cech; Bellerin, Koscielny, Monreal (Mustafi 46), Maitland-Niles; Wilshere, Xhaka, Ozil; Iwobi (Welbeck 78), Lacazette, Sanchez (Walcott 89).
Subs not used: Ospina, Kolasinac, Elneny, Coquelin.
Bookings: Iwobi.
Goals: Sanchez 53, Xhaka 56, Ozil 58.


Liverpool (4-3-3): Mignolet; Gomez, Lovren, Klavan, Robertson; Can, Henderson (Milner 11), Coutinho (Oxlade-Chamberlain 84); Salah, Firmino, Mane (Wijnaldum 80).
Subs not used: Karius, Alexander-Arnold, Lallana, Solanke.
Goals: Coutinho 26, Salah 52, Firmino 71.
Referee: Martin Atkinson.  
Attendance: 59,409











Wednesday, December 20, 2017

Mawingu Tz

Matokeo Mechi Za Jana Kombe La CARABAO CUP Nchini Uingereza

Man city Wameshinda Kwa Mikwaju ya penalt..timu Hizo Zimetinga Nusu Fainal

Sunday, December 17, 2017

Mawingu Tz

Man City Haikamatiki, Yaipiga Tottenham Hotspur Mabao 4-1

Kevin De Bruyne katikati akishangilia na wenzake.
NI kama haina mpinzani katika Ligi Kuu ya England kwani Manchester City jana usiku iliifunga Tottenham Hotspur mabao 4-1 na kujiimarisha kileleni mwa Premier League.

Ushindi huo umeifanya Man City inayonolewa na Pep Guardiola kufikisha pointi 52 huku anayefuatia Manchester United akiwa na pointi 38. Man United leo inacheza na West Brom katika ligi hiyo. Spurs imebaki na pointi 31 na imeshuka hadi naafsi ya saba.
Mabao ya Man City yalifungwa na Ilkay Guendogan dakika ya 14 baada ya kupokea pasi ya Leroy Sane huku bao la pili likifungwa na Kevin De Bruyne akimalizia pasi ya Guendogan. Bao la tatu lilifungwa na Raheem Sterling dakika ya 80, Sterling alifunga bao la nne dakika ya 90. Spurs ilipata bao lake dakika ya 90 mfungaji akiwa ni Christian Erikssen


Gabriel Jesus akijiandaa kuingia Uwanjani.
Man City imeendeleza rekodi ya kutofungwa msimu huu kwani hadi sasa imecheza mechi 18 ambapo imeshinda mara 17 na kutoka sare mara moja.
MSIMAMO TOP FIVE PREMIER
P W D L Pts
1.Man City 18 17 1 0 52
2.Man United 17 12 2 3 38
3.Chelsea 18 12 2 4 38
4.Arsenal 18 10 3 5 33
5.Burnley 18 9 5 4 32

Tuesday, December 12, 2017

Mawingu Tz

Haya Hapa Makundi Kombe La Mapinduzi...Singida UTD Yaongezwa...Mtibwa OUT

MPYA : Makundi kombe la Mapinduzi 2017
Makundi kombe la Mapinduzi 2017 leo yametangazwa huku Simba na Azam wakijikuta kwenye Kundi Moja na Wageni Waalikwa URA kutoka NCHINI Uganda.
Katika Kundi A Kuna Timu za Azam Fc (Mabingwa watetezi) , Jamhuri , Mwenge, Simba Na URA kutoka Uganda.
Kundi B Lina timu za Yanga, JKU, Mlandege Fc. Singida United, Taifa Jang’ombe na Zimamoto.
Kamati itakutana kupanga ratiba kamili na leo ilikuwa siku ya Kutangaza Makundi tu
“Tunataraji kutoa ratiba rasmi ya mashindano hayo hivi karibuni, kwani hivi sasa tunakamilisha hatua za mwisho ambapo kina jambo dogo tu limejitokoeza ndio maana tumechelewa ila ratiba itatoka mapema,”
Alisema baada ya Kutangaza makundi hayo moja kati ya wajumbe wa kamati ya Mashindano hayo, Kama kawaida kwataunit.com tutakuwa nawe sambamba kukupa kila linalohusu Mashindano haya.