Showing posts with label KITAIFA. Show all posts
Showing posts with label KITAIFA. Show all posts

Friday, January 12, 2018

Mawingu Tz

Ajibu Aomba Radhi Yanga

Mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu.
BAADA ya kipigo cha penalti 5-4 dhidi ya URA, juzi mshambuliaji wa Yanga, Ibrahim Ajibu Migomba ameom­ba radhi kwa mashabiki wa timu hiyo kuto­kana na ma­tokeo ma­baya.

Yanga ilion­dolewa kwenye michuano ya Kombe la Map­induzi katika hatua ya nusu fainali na URA ya Uganda kutinga fainali dhidi ya Azam FC.

Msham­buliaji huyo alisema hawakupenda kupata matokeo ya aina ile lakini ilitokea vile kwa sababu mpira una matokeo matatu.

“Naomba mashabiki wetu wa Yanga wa­tusamehe kwa matokeo mabaya hakuna timu ambayo inapenda kupoteza zaidi mtupe sapoti ,”al­isema Ajibu.

Hata hivyo katika mchezo huo wachezaji ambao wali­piga penalti ni Papy Tshishim­bi, Hassan Kessy, Gadiel Michael, Daud Raphael na Obrey Chirwa ambaye alikosa.
Mawingu Tz

Mzee Akilimali Aingilia Ishu Ya Chirwa

Ibrahim Akilimali.
MWENYEKITI wa Baraza la Wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali amemtetea mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa kufuatia kukosa penalti katika mechi ya juzi dhidi ya URA ya Uganda kwenye Kombe la Mapin­duzi.

Yanga iliondolewa katika nusu fainali kwa penalti 5-4 ambapo Chirwa alikosa kwa upande wa Yanga na kusaba­bisha kuwa gumzo kutokana na tukio hilo.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Akilimali alisema Chirwa hakufan­ya makosa katika kupiga penalti ya mwisho kwani alidhamiria kufunga na kilichotokea ni bahati mbaya na kudai kuwa, kocha ndiye anayepaswa kulaumiwa kutokana na kumtumia licha ya kutokuwa na ma­zoezi ya pamoja na wenzake.

“Yanga tumetolewa kiume katika michuano ya Mapinduzi kwani hadi tunatoka tumefanikiwa kufanya vyema hadi dakika 90 lakini kili­chotokea hakipaswi kulaumiwa mchezaji.

“Timu ilicheza vizuri ilipamba­na na hatimaye kuweza kufikia hapo tulipofikia na ilikuwa ni lazima timu moja isonge mbele.

“Siwezi kumlaumu Chirwa, kilichotokea ni bahati mbaya kwani, hata wachezaji wa­zuri Ulaya wanakosa penalti sembuse yeye, anayepaswa kulaumiwa ni kocha kwanini amemchezesha mchezaji akiwa hana mazoezi, naona anayarudia yaleyale ya Kocha Hans Pluijm,” alisema Akilimali.

Thursday, January 11, 2018

Mawingu Tz

Rage Aipa Makavu Simba Na Awapa Ujumbe Huu Mzito Kuhusu Suala La Ubingwa Wa Ligi

Ismail Aden Rage.
ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Simba, Ismail Aden Rage, ameibuka na kusema kuwa, ndani ya klabu hiyo kuna tatizo na kama hawa­takuwa makini, basi kuna uwezekano hata ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu timu hiyo ikauokosa.

Rage ameyasema hayo kufuatia Simba, Jumatatu kuondoshwa kwenye Kombe la Mapinduzi, huku pia ikiwa imeshaondolewa kwenye Kombe la FA.

Rage amesema licha ya Simba kuwa vinara wa ligi kwa sasa, lakini kama viongozi, wachezaji na benchi la ufundi hawatakuwa na umoja, timu itavurugana zaidi na kushindwa kufikia malengo.
“Ukiangalia Simba ya msimu huu naona kama imerudia makosa ya Yanga waliyowahi kuyafanya huko nyuma, wamesajili wachezaji wengi bila ya kuangalia uhitaji wa timu zaidi ya kuangalia majina tu. Hili ni tatizo.

“Tatizo lingine ninaloliona ndani ya Simba mpaka kusababisha kufanya kwao vibaya ni kutokuwa na umoja baina ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi, wanatakiwa kukaa chini na kumaliza tofauti zao haraka kabla hatari zaidi haijatokea. Kugombana kumepitwa na wakati.

“Haiwezekani leo hii eti wachezaji wanafanyiwa mabadiliko halafu wanaondoka kwenye benchi, huu ni utovu wa nidhamu. Nawasihi wote kwa pamoja wakae chini wamalize tofauti zao wafanye kazi kwani wana kikosi kizuri lakini mambo madogomadogo kama hayo ndiyo yanawasumbua,” alisema Rage.

Tuesday, January 9, 2018

Mawingu Tz

Alichosema Masoud Djuma Baada Ya Kina Mkude Na Kichuya Kutoonekana Benchi...


Alichosema Masoud Djuma baada ya kina Mkude na Kichuya kutoonekana Benchi baada ya kufanyiwa sub.
Jana story kubwa ilikuwa ni Simba kutolewa michuano ya Mapinduzi lakini story nyingine ikaibuka katikati yake kufuatia baadhi ya wachezaji wa Simba kutoonekana katika benchi mara baada ya kutolewa(Kufanyiwa sub) na badala yake kuonekana wamekaa maeneo mengine kabisa ya uwanja wakifatilia mechi.
Masoud Djuma msomaji  ni kocha msaidizi anayeiongoza Simba amewatetea kina Mkude na Kichuya kwa kusema kuwa yeye ndiye aliyewaruhusu wachezaji hao kuondoka katika benchi mara baada ya kuwafanyia mabadiliko.
Masoud amesema wachezaji hao walikuwa wamechoka na hivyo aliwaruhusu waende wakafanyiwe massage vyumbani na hakukuwa na ulazima kwa wao kurejea benchi na wala siyo Tatizo la Nidhamu kama ambavyo wengi walitafsiri.
Katika mchezo huo kati ya Simba na URA kutoka nchini Uganda Simba ilifanya mabadiliko kwa kuwatoa wachezaji Shiza Kichuya, Nicolas Gyan, Jonas Mkude, Mzamiru Yassin na Mwinyi Kazimoto na nafasi zao kuchukuliwa na Mo iBRAHIM, James Kotei, Yusuph Mlipili, Laudit Mavugo na Said Hamis Ndemla.
Simba katika mchezo huo alihitaji ushindi ili kujihakikishia kufuzu katika hatua ya nusu Fainali ya michuano hiyo ya Mapinduzi lakini aliishia kufungwa bao moja pekee bao likipatikana kipindi cha kwanza mara baada ya mchezaji Deboss Kalama kuwahadaa mabeki wa Simba na Kuachia Shuti kali lililomshinda kipa Emmanuel Mseja.
Nusu Fainali zitachezwa kesho Jumatano kati ya Yanga na URA na Azam na Singida United katika uwanja wa Amani Zanzibar.


Mawingu Tz

Chirwa Ang’oa Kigogo Yanga


SUALA la fungu lililobaki la usajili wa straika wa Yanga, Obrey Chirwa, limechukua sura mpya baada ya kigogo mmoja wa klabu hiyo kuamua kuachia ngazi, huku baadhi wakidai kuwa kigogo huyo ameamua kufanya hivyo kuepuka lawama.
Chirwa ambaye aliripotiwa kuomba ruhusa ya kwenda kwao Zambia kwa ajili ya matatizo yake ya kifamilia, lakini baadaye ilidaiwa amegoma kurejea Jangwani, akiwashinikiza mabosi wa Yanga kummalizia fedha zake za usajili.
Imedaiwa kuwa sababu ya straika huyo ‘kususa’ kurejea nchini ni kutokana na mvutano kati ya mchezaji huyo na uongozi wa klabu ambao unadaiwa kushindwa kummalizia fungu lililobaki kutokana na baadhi ya wajanja wachache kugawana kinyemela.
Habari zinasema wakati nyota huyo anasajiliwa mwaka 2016, tayari alishatengewa Dola 100,000 (zaidi ya Sh milioni 200 za Tanzania), lakini sehemu ya fedha hizo zilichotwa na wapiga dili.
Ni kutokana na mkanganyiko huo, inaelezwa kwamba tayari kigogo mmoja wa Yanga ameandika barua ya kuuacha wadhifa wake, sababu ikitajwa kuwa ni baada ya baadhi ya watu kumshutumu kuhusika na sakata la Chirwa.
DIMBA lilimtafuta Katibu Mkuu wa klabu hiyo, Charles Boniface ‘Mkwasa’, ili kuthibitisha suala hilo lakini akasema hana taarifa hizo, japo taarifa kutoka Yanga zinadai kuwa ni kweli yupo kigogo aliyeamua kuachia ngazi.
“Siwezi kuthibitisha juu ya suala hilo kwa kuwa sijapata barua yoyote kutoka kwa kiongozi yeyote kujiuzulu na mimi juzi nilikuwa ofisini mpaka usiku,” alisema Mkwasa.
Akizungumzia kuhusu tetesi hizo za baadhi ya wajanja kumega fedha za Chirwa, Mkwasa alisema hana uhakika ila anachojua yeye ni kwamba mchezaji huyo ana madai yake na wanafanya taratibu za kumlipa.
Alipoulizwa juu ya ujio wa mchezaji huyo, Mkwasa alisema tayari yupo nchini tangu juzi usiku na sasa wanafanya jitihada za kumaliza tatizo lake ili aweze kujiunga na wenzake kwa ajili ya maandalizi ya michuano mbalimbali.
Kwa mujibu wa habari za ndani, Yanga walikuwa wanahaha kuhakikisha kuwa mchezaji huyo anarejea nchini, baada ya kumwambia kuwa madai yake yote yataisha baada ya yeye kuwasili nchini.
Taarifa zaidi kutoka Yanga zinadai kuwa mzigo mkubwa kwa sasa umemwelemea Mkwasa kwani anafanya kila linalowezekana kuhakikisha wachezaji wanalipwa mishahara yao huku ikidaiwa kuwa wapo wajanja wachache walioifanya klabu hiyo kuyumba.
Mawingu Tz

Niyonzima Arejesha Matumaini Simba

WAKATI wenzake wakiwa kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi huko visiwani Zanzibar, kiungo mchezeshaji wa Simba, Mnyar­wanda, Haruna Niyonzima yeye yupo jijini Dar es Salaam akiendelea kujifua ufukweni.
Mnyarwanda huyo alibaki Dar ku­tokana na majeraha ya enka anayoen­delea kuyauguza yaliyomuweka nje ya uwanja kwa muda wa wiki mbili.
Kiungo huyo, alipata majeraha hayo akiwa kwenye mazoezi ya timu hiyo wakati kikosi hicho kikiwa na Mcam­eroon, Joseph Omog aliyesitishiwa mkataba wake hivi karibuni kabla ya msaidizi wake Mrundi, Masoud Djuma kukabidhiwa.
Akizungumza na Championi Ju­matatu, Niyonzima alisema ameanza programu hiyo ya kukimbia ufukweni kwa ajili ya kuiponyesha enka hiyo ili ipone kabisa.
Niyonzima alisema, wakati akien­delea na matibabu mengine atafanya mazoezi ya ufukweni kwani mchanga ni sehemu ya tiba kwa ajili ya jeraha hilo la enka linalomsumbua.
Aliongeza kuwa, hataki kuona akiendelea kusumbuka na jeraha hilo ambalo mara kwa mara linamtokea ili atakaporejea uwanjani lisijirudie.
“Mimi nipo Dar na sipo na timu Zan­zibar, kama unavyofahamu bado enka inanisumbua na hivi sasa nipo nafanya mazoezi ya kukimbia ufukweni huku nikiendelea kupata matibabu mengine hospitali.
“Na mazoezi haya ya ufukweni nayo ni sehemu ya tiba kwangu, kwani mchanga nao ni tiba kwa jeraha hili la enka inayonisumbua kwa muda mrefu,” alisema Niyonzima aliyetua kuichezea Simba katika msimu huu.