Tuesday, December 26, 2017

Mawingu Tz

Mtoto Wa Lwandamina Alikunywa Sumu Baada Ya Tukio Hili La Kusikitisha


Mtoto wa Lwandamina alikunywa Sumu baada ya Tukio hili la Kusikitisha
Wakati wanachama, washabiki na wapenzi wa Yanga wakimsubiri kocha wao George Lwandamina kurejea Yanga kuendelea na Majukumu yake walipokea taarifa kuwa kocha huyo amefiwa na mwanaye Copa Mofya Lwandamina aliyedaiwa kufa kwa Kunywa Sumu.
Kupitia mtandao wa Futaa Zambai umeeleza Chanzo cha Kifo cha Mtoto wa Lwandamina Copa.
Inadaiwa siku ya tukio Copa (Mtoto wa Lwandamina) akiwa na rafiki yake Keith Chemu walikuwa wamekunywa pombe na Kulewa ndipo walimvaa mpangaji wa nyumbani kwao Aliyejulikana kwa jina la Hellen.
Walimvamia na Kumbaka na Kisha kumwibia simu na kiasi cha Shilingi 90000 za Kitanzania na wakampiga wakijua wameshamuua.
Baada ya muda mtoto wa Lwandamina alipata taarifa kuwa binti huyo mwenye Miaka 25 alikuwa hajafa na alikuwa hospitali na taarifa zilikuwa zishafika polisi na punde angeanza kutafutwa.
Hali ya taarifa hiyo ilimfanya Copa Lwandamina miaka 28 kuogopa na kuamua kuchukua maamuzi ya Kunywa Sumu.

Rafiki yake Keith Chemu waliyefanya naye tukio  kwasasa anashikiliwa na jeshi la polisi huko Lusaka Zambia katika jela ya Godfrey Chitalu akiwa kama Mahabusu kwa kosa la Kubaka na kujaribu kuua.
Hata hivyo inaelezwa kuwa hali ya binti Hellen  aliyekuwa na hali mbaya akiwa na alama shingoni na maumivu ya maeneo mengine kutokana na kupigwa inaelezwa kuwa anaendelea vizuri.

Tupe Maoni Yako