Wednesday, December 13, 2017

Mawingu Tz

Himid Mao Mbioni Kumalizana Na Timu Hii Ya Afrika Kusini

Wakati dirisha dogo la usajili likielekea kufungwa siku chache zijazo, kuna taarifa kadhaa kuhusu usajili wa wachezaji wa Tanzania.
Inadaiwa kuwa kiungo mkabaji wa Azam FC, Himid Mao, amefuzu majaribio ya kujiunga na Klabu ya Bidvest inayoshiriki Ligi kuu ya nchini Afrika Kusini na yuko mbio kwenda kumalizana naoHimid Mao – Tanzania.
Bado hakuna taarifa kamili kutoka Azam FC juu ya taarifa hizo za usajili.
Aidha, upande mwingine inaelezwa kuwa Muhsin Makame ambaye ni mshambuliaji wa Serengeti Boys amejiunga na Njombe Mji kwa mkopo akitokea Klabu ya Mtibwa Sugar ya mkoani Morogoro.

Tupe Maoni Yako