Monday, December 11, 2017

Mawingu Tz

Simba Vipi Kuhusu Yule Striker Wa Rayon Sports? Ishu Imekaa Hivi


Baada ya Simba kuhusishwa na kutaka kumsajili Mrundi, Nahimana Shassir anayeichezea Rayon Sport, dili hilo limekufa rasmi baada ya Kocha Msaidizi wa Simba, Masoud Djuma kusema hawatamsajili.

Djuma ambaye ni raia wa Burundi, alipendekeza kusajiliwa kwa mchezaji huyo, lakini baada ya kumuangalia zaidi, amejiridhisha kwamba hata akija hatakuwa na msaada wowote.

Djuma amesema: “Nilipendekeza asajiliwe lakini mpaka sasa tumesitisha dili hilo kwa sababu ameshuka kiwango, nimemuangalia kwenye michuano ya Chalenji nimeona hajaisaidia chochote timu yake, hivyo hatutamsajili tena.

“Hatuwezi kumsajili mchezaji wakati uwezo wake ni mdogo kuliko wale waliopo ndani ya kikosi chetu cha sasa.”

Tupe Maoni Yako