Tuesday, December 19, 2017

Mawingu Tz

Azam Fc Yaweka Sawa Kuhusiana Na Mbaraka Yusuf Kuumia Timu Ya Taifa





Klabu ya Azam FC imesema mshambuliaji wao, Mbaraka Yusuf amegundulika ana tatizo la mfupa laini wa goti.

Msemaji wa Azam FC, Jaffar Iddi Maganga amesema, Mbaraka amegundulika ana tatizo hilo la Meniscus baada ya kufanyiwa vipimo akiongozwa na daktari wa klabu hiyo, Juma Mwankemwa.

“Kwa hiyo matibabu yanaendelea na klabu ya Azam FC ndiyo inayoshughulikia, hivyo suala la kwamba ametelekezwa, hapana,” alisema.


Mbaraka aliumia wakati akiitumikia timu ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars katika michuano ya Chalenji iliyomalizika kwa wenyeji Kenya kubeba kombe dhidi ta Zanzibar Heroes kutoka Tanzania.

Tupe Maoni Yako