Wednesday, December 27, 2017

Mawingu Tz

Kocha Morocco wa "Zanzibar" azungumzia tetesi za Kutua Yanga,Vipi Stars?

Kocha Mkuu wa ” Zanzibar Heroes ” Hemed Morocco ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kufuatia soka safi la timu yake ya Taifa ya Zanzibar akisimama kama kocha mkuu kwenye timu hiyo ya Taifa.
Kwasasa kulikuwa na tetesi mbili kubwa zikimhusisha Hemed Morocco moja ikiwa ya nje ya nchi na nyingine ikiwa ni ya Hapa Hapa Tanzania.
Ya Nje ya Nchi msomaji wa Kwataunit.com ni ile ya kufundisha soka katika timu ya taifa ya Sudani Kusini na ya Ndani ikitajwa kuwa ni ya Yanga.
Akiongelea kama kuna timu yoyote imeshamfata nchini (Tanzania) Hemed Morocco amesema Hakuna timu iliyomfata na kufanya naye mazungumzo Tanzania mpaka sasa.
Na Kuhusu Sudan Kusini.
Morocco amesema ni kweli Sudan Kusini viongozi wa timu hiyo ya taifa walimfata wakati wa michuano ya CECAFA na wakafanya naye mazungumzo kuhusu uwezekano wa yeye kwenda kufundisha soka Sudan Kusini.
Amesema kuwa baada ya kumfata walifanya mazungumzo naye ya awali lakini mpaka sasa hakujawa na mawasiliano serious lakini kama wakitaka kufanya naye kazi yeye yuko tayari kwenda kwani kwasasa anatamani kufanya kazi Nje ya Nchi.
Morocco msomaji wa Kwataunit pia amewahi kuifundisha Stand United akiliongelea suala la Kama yupo tayari kufundisha Taifa Stars amesema kwasasa hawezi kuongelea suala hilo.


Tupe Maoni Yako