Tuesday, January 9, 2018

Mawingu Tz

Manara Alia Na Mapinduzi Cup Ashindwa Kujizuia, Atoa Mazito.

Baada ya klabu ya Simba kupokea kipigo cha pili katika michuano ya kombe la Mapinduzi kutoka kwa watoza Ushuru wa Uganda ( URA) Cha goli 1-0 Afisa habari wa klabu hiyo,Haji Manara amesema hana neno linaloweza kutosha kuelezea kilichotokea uwanjani.
Aidha amesema kuwa anayajua maumivu wanayopata mashabiki wa timu hiyo kwani yeye ni Msemaji lakini shabiki wa klabu hiyo.
“Kila sentesi niliyoandika nimefuta, hakuna neno linalotosha kuelezea hisia zangu kwa kilichotokea leo Amaan Stadium..nayajua maumivu ya wanasimba….shida yangu mimi ni msemaji kisha shabiki wa hii timu..najua sana pain yenu…but lazma maisha yasonge mbele…
🙏🙏
”>>>Manara



Tupe Maoni Yako