Monday, January 8, 2018

Mawingu Tz

Kamusoko Aendelea Na Mazoezi Dar, Moja Ya Kazi Ni Kupunguza Uzito

Kiungo Thabani Kamusoko ameendelea na mazoezi ya kurudi fiti ikiwa ni pamoja na kupunguza uzito.

Kamusoko ambaye alianza mazoezi taratibu wakati Yanga ikijiandaa na kwenda katika michuano ya Mapinduzi, moja ya sharti alilopewa ni kupunguza uzito.

"Kamusoko yuko Dar es Salaam, anaendelea na mazoezi mbalimbali yakiwemo ya kupunguza uzito, tukirejea tunaweza kuungana naye," alisema mmoja wa viongozi.

Kiungo huyo amekuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi miwili na ushee akiuguza maumivu ya goti lake.

Tupe Maoni Yako