Saturday, December 23, 2017

Mawingu Tz

USAJILI : Mido La Kutisha Lililoyetinga "first eleven" CECAFA Laitaja Yanga

USAJILI : Aliyetinga ” first eleven ” CECAFA aitaja Yanga
Kiungo wa timu ya Taifa ya Zanzibar ” Zanzibar Heroes ” Abdulaziz Makame amefunguka Juu ya kama Yanga wanamwitaji kumsajili na Kusema yeye yuko tayari.
Makame aliyeng’ara sana kwenye michuano ya CECAFA yaliyofanyika mapema mwezi Huu (December ) nchini Kenya katika miji ya Machakos na Kisumu kiasi cha kuvutia timu nyingi
Makame msomaji wa Kwataunit.com amesema yeye yuko tayari kucheza Yanga na kama kweli Yanga wanamtaka basi hata leo hii yeye yuko tayari kucheza timu hiyo.
Abdulaziz Makame alikuwa moja kati ya wachezaji waliochaguliwa kwenye kikosi bora cha mashindano ya CECAFA 2017 kutokana na kucheza mechi zote katika ubora wa hali ya Juu.
Hata hivyo katibu mkuu wa Yanga Boniface Mkwasa siku kadhaa zilizopita aliiambia kwataunit.com kuwa baada ya kumsajili Mkomola na Kayembe hawana mpango wa Kuongeza mchezaji mwingine ndani ya Kikosi chao.

Tupe Maoni Yako