Sunday, December 10, 2017

Mawingu Tz

Kamusoko Bado Bado Yanga

Kiungo wa Yanga, Thabani Kamusoko ataendelea na matibabu na hatatakiwa kuanza mazoezi ndani ya siku 7 zijazo.

Mmoja wa viongozi wa Yanga amesema juhudi za kumtibu zinaendelea, lakini inaonekana atatakiwa kuwa na muda wa kusubiri.

Uongozi wa Yanga na wanachama na mashabiki wake wamekuwa wakifanya juhudi kubwa kuhakikisha Kamusoko anarejea uwanjani.

Kiungo huyo mwenye nidhamu asiye na makuu, pamoja na kuwa mgonjwa amekuwa akijitokeza uwanjani wakati wenzake wakifanya mazoezi.

Tupe Maoni Yako