Wednesday, December 6, 2017

Mawingu Tz

Taarifa Mpya Kutoka Yanga Asubuhi Ya leo Kuhusu Ngoma Kuzuiwa Kufanya Mazoezi Na Adhabu Atakayopewa

Huku wachezaji wenzake wakianza mazoezi ya pamoja kwa ajili ya mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbao, mshambuliaji wa Yanga Mzimbabwe, Donald Ngoma yeye amepigwa ‘stop kuungana nao.
Hiyo, ikiwa ni siku chache tangu mshambuliaji huyo aliporejea nchini akitokea nyumbani kwao Zimbabwe alipokwenda kujitibia bila ya ruhusa ya viongozi.

Timu hiyo, imeanza mazoezi hayo juzi Jumatatu kwenye Gym ya City Mail iliyopo Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam chini ya kocha msaidizi, Shadrack Nsajigwa.

Taarifa zinaeleza, mshambuliaji huyo amezuiwa kuanza mazoezi hadi pale itakapotolewa hukumu ya adhabu yake kutokana na kosa la kinidhamu alilolifanya.

Mtoa taarifa huyo alisema, kamati ya utendaji ya timu hiyo hivi sasa inafanya vikao vyake kwa ajili ya kujadili adhabu ipi anayotakiwa kupewa mshambuliaji huyo baada ya kutenda kosa hilo.
 “Ngoma tumemzuia kwa hivi sasa kujihusisha na chochote katika timu ikiwemo kufanya mazoezi ya pamoja na wenzake walioanza gym, juzi Jumatatu asubuhi.

“Hivyo, mshambuliaji huyo tumemzuia kuanza mazoezi ya gym ambayo alitakiwa kuanza na wenzake kwa ajili ya kujiandaa na mechi ijayo ya ligi kuu dhidi ya Mbao FC.

“Tunataka nidhamu katika timu na kamwe hatutasita kutoa adhabu kwa mchezaji yeyote atakayekwenda kinyume na nidhamu kama ilivyokuwa kwa Ngoma ambaye yeye ligi kuu ikiendelea aliondoka kimyakimya nchini na kuelekea nyumbani kwao Zimbabwe,”alisema mtoa taarifa huyo.

Taarifa nyingine za mshambuliaji huyo za kukabidhi ripoti ya daktari wake aliyekuwa anamtibia Zimbabwe inayomtaka kupumzika nje ya uwanja kwa muda wa wiki sita.

Katibu Mkuu wa Yanga, Boniface Mkwasa amethibitisha kurejea kwa mshambuliaji ambaye aliondoka bila kutoa taarifa na amesema kwamba, maelezo na ripoti aliyokuja nayo bado hayajitoshelezi.


“Bado maelezo hayajitoshelezi kwa maana ya kwamba, ripoti imeandikwa na daktari wake lakini baada ya kutafakari tunahitaji tupate ripoti kamili kutoka kwa daktari wetu.


Tupe Maoni Yako